May 17, 2013

DIWANI WA CCM KATA YA TITU KILOLO AFARIKI DUNIA

Chama  cha mapinduzi (CCM) wilaya ya  Kilolo  mkani Iringa  kimpata  pigo  kubwa  kufuatia  kifo cha  diwani  wake wa kata ya Mtitu Marehemu  Checo Ngimba.
 
Taarifa  ambazo mtandao  huu  wa  www.matukiodaimacom ambazo uezipata  ziadai  kuwa  diwani  huyo amefia katika Hospitali ya Ikonda  wilaya ya Makete na leo amezikwa  katika kata  hiyo ya Mititu.

AEMAVYO MBUGE ZITTO KABWE LEO ........

Draft 3- The Natural Gas Policy of Tanzania -2013to be presented to MPs tomorrow
 
Kesho jumamosi wabunge tumealikwa kwenye semina kuhusu sera ya Gesi Asilia. Tumegawiwa tayari nakala zetu, tena zipo kwenye lugha ya kimombo.
Ikumbukwe kwamba kuanzia tarehe 22 - 23 Mei 2013 kutakuwa na mjadala wa bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini. Semina hii ni maandalizi ya Bajeti hii.
Jambo la kushangaza ni kwamba wakati sera ya Gesi Asilia ipo kwenye rasimu na ndio kwanza wabunge tumeletewa kutoa maoni, Serikali tayari imetangaza tena kugawa vitalu vya Mafuta na Gesi kwenye Bahari kuu na Ziwa Tanganyika Kaskazini.
Zabuni hii mpya ya vitalu vya utafutaji imetolewa wakati kuna maamuzi ya Bunge kuzuia ugawaji huu mpya mpaka sera ya Gesi Asilia na Sheria ya Gesi vikamilike.
Haraka hii ya serikali kugawa vitalu bila sera wala Sheria inatoka wapi? Nitashangaa sana wabunge kukimbilia posho za semina hii na kuhalalisha maamuzi yasiyo zingatia maslahi ya Taifa Kwa vizazi vya sasa na vijavyo. Uamuzi wa kugawa vitalu vipya bila kwanza kuwepo Kwa sera na Sheria mpya unapaswa kupingwa Kwa Nguvu zote.
Tafuta mbunge wako, mwambie asikubali maamuzi haya ya serikali.
Tumalize kwanza sera na Sheria ndio tugawe vitalu vipya. Gesi sio viazi, haiozi.
Naomba tureje statement yangu ya mwaka jana September 2012:
Oil and Gas in Tanzania: Building For A Sustainable Future
A Call for a moratorium on new offshore exploration.
Tanzania is on the precipice of an economic evolution with the recent discoveries of gas.
  We have now confirmed reserves of 43 Trillion Cubic feet (TCF), roughly valued at USD 430bn[i]. Plans for LNG production are moving ahead of schedule.
 
As a result there will be considerable new gas resources available for power generation and other needs for our economy and people including domestic use, petrochemical industries and fertilizer plants.


Our nascent oil and gas industry is set to expand greatly with the upcoming Fourth Licencing Round, which, according to Minister Sospeter Muhongo, is scheduled to be launched in Houston, Texas on September 13. We are now informed that the licencing round has been delayed. This is not enough and more work needs to be done.
The Fourth Licencing Round should be put on hold – postponed for ten years. In this, we echo the demand of Parliament’s Energy and Minerals Committee earlier this year (April 2012, Annual Report of the Committee) and the concerns of other informed citizens.
 
 It is very unfortunate that the recommendation to postpone the licensing round, supported by a Parliamentary Committee on Public Investments (POAC) and approved by a Parliamentary resolution, was largely ignored by the Ministry and TPDC.
 
A moratorium will not only allow us to manage our new resources effectively it will also ensure the welfare of future generations. This is something the Government must take seriously.
We, as responsible leaders, have a duty to safeguard this country’s resources for future generations. This will require effective and sustainable management of our oil and gas reserves. The licencing round for the oil and gas offshore blocks announced by the Ministry through TPDC undermines our mandate to the Tanzanian people. If all exploration blocks are being licenced, what will our grand-children and great-grandchildren, who will be more educated and well prepared, do? It is critical that we approach these issues not in a short-term strategic thinking but long-term. We may not be here tomorrow but Tanzania will be.
We are not prepared for an expansion of exploration activity. Current legislation is out-dated and does not mirror the current political and economic status quo.
 
  We have no overarching Gas Policy, however progress has been made as both the Gas Act and Policy are currently being crafted.
 
 Nevertheless to continue on with a new round of licensing before these policies are complete is irresponsible. More importantly, we do not have legislation that will manage revenues from the sector.
We need more time for the policies and legislative acts to be implemented. We will also need more time for institutions to be in place.
A ten-year moratorium will give us the space to develop our capacity in key areas. TPDC can be overhauled to become an active exploration and production company, modelled on Malaysia’s Petronas. Currently, TPDC does not have the capacity or resources to be an effective and strong partner in developing our reserves. These capacity deficits include the ability to conduct basic geological surveys, contract negotiations and management as well as production and processing.
A moratorium will allow us to support TPDC to become a strong and reliable trustee and gatekeeper of the country’s resources.
A ten-year moratorium will allow us to build the necessary institutions that we will need to effectively benefit from these resources. These include establishing and supporting a Sovereign Development Fund , to manage revenues; coordinating with our educational institutions to train and foster young Tanzanians so they can confidently work and engage in this industry; and an oversight committee that would include parliamentarians, civil society organizations and local communities. These stakeholders would be mandated to ensure that our resources are used effectively and fairly.
A ten-year moratorium on offshore exploration will ensure that our increasingly young population will enjoy the benefits of our natural resources for generations to come. We kindly request the Government to stop any new licencing of exploration blocks and refocus all efforts into building the capacity to manage the discovered resources, make wise decisions and prepare the nation for a Natural Gas Economy in a timely manner.
Our past mistakes in the mining sector should guide us, as we comprehend the challenges and opportunities presented by the oil and gas sector. The country must first build strong accountability measures, ensure transparency, develop critical human capital and learn from case studies of other gas economies before licencing any new blocks. We need to think strategically and understand the long-game rather than thinking about short-term gains. As a result, we think 10 years will be enough to implement the necessary interventions and build a strong and sustainable oil and gas economy for all Tanzanians.
Kabwe Zuberi Zitto, MP

WANAFUNZI 15 WAKAMATWA NA POLISI MBEYA

RPC  Mbeya Diwani Athuman
Na Esther Macha, Mbeya

WANAFUNZI kumi na tano(15) katika shule ya sekondari ya Wazazi ya Lupata Wilayani Rungwe Mkoani Mbeya wanashikiliwa na jeshi la polisi kwa kosa la kuchoma moto bweni la shule hiyo kutokana na wanafunzi wenzao kusimamishwa masomo  na uongozi wa shule kwa utovu wa nidhamu.

Akizungumza na waandishi wa habari jana ,Kamanda wa polisi Mkoani Mbeya Bw.Diwani Athuman alisema kuwa tukio lilitokea mei 14 mwaka huu majira ya saa 2.00 usiku katika shule ya sekondari Lupata.

Bw.Athuma alisema kuwa wanafunzi hao baada ya kuona wanafunzi wenzao watatu wamesimamishwa  masomo walianza  vurugu usiku na kuanza kuchoma moto  bweni moja  la wanafunzi wa kiume .

Aidha Kamanda Athuma aliwataja wanafunzi waliosimamishwa kwa utovu wa  nidhamu shuleni hapo kuwa  ni ,Joseph Robert (18) Kidato cha nne Mkazi wa Kitunda Jijini Dar es Salaam,Mwita Chacha(17),Mwanafunzi wa  kidato cha tatu  mkazi wa Jijini Dar es Salaam ,pamoja  na Daniel David(18)kidato cha Tatu mkazi wa Ipinda Kyela.

 “Hawa wanafunzi watatu waliosimamishwa masomo walihamasisha wenzao kuunga mkono kupinga adhabu hiyo  kwa kufanya  vurugu na kuchoma bweni hilo la wanafunzi”alisema Kamanda Athuman.

Alisema kuwa  bweni lilochomwa moto walikuwa wanaishi wanafunzi ambao hawakuwa tayari  kuunga mkono uvunjifu huo wa amani shuleni hapo.

Aidha Bw. Athuman alisema kuwa kufuatia  vurugu hizo vinara wawili wa vurugu hizio wanashikiliwa na jeshi kwa mahojiano zaidi ambao ni ,Joseph Robert , Mwita Chacha huku  watuhumiwa kumi na tano wanashikiliwa na jeshi hilo.

Kuhusu vitu ambavyo vimeharibiwa Kamanda huyo alisema thamani halisi ya uharibifu uliotokea bado kujulikana na kwamba hakuna madhara yeyote ya kibinadamu  yaliyotokea .

Hata hivyo Bw.Athuman ametoa wito kwa jamii  hasa wanafunzi kuacha tabia  ya kujichukulia sheria mkononi kwani ni kinyume cha sheria na badala yake watatue matatizo  kwa njia ya meza ya mazungumzo katika mamlaka husika ili kuepusha madhara na hasara zinazoweza kujitokeza ambazo mara nyingi wahanga wanakuwa ni wanafunzi wenyewe.

 Mwisho.

PAZIA LIGI KUU YA VODACOM KUFUNGWA JUMAMOSI NI TAARIFA KUTOKA TFF LEO


Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara msimu huu (2012/2013) inafikia tamati kesho (Mei 18 mwaka huu) kwa timu zote 14 kupambana katika viwanja saba tofauti.  

Mechi zote zitachezwa kuanzia saa 10 kamili jioni. Ni jukumu la kamishna wa mechi husika kuhakikisha mchezo unaanza katika muda uliopangwa, vinginevyo hatua za kinidhamu zitachukuliwa kwa mujibu wa Kanuni za Ligi Kuu ya Vodacom toleo la 2012.
Yanga ambayo tayari imeshatwaa ubingwa itakuwa mgeni wa Simba katika mechi namba 180 itakayochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo mwamuzi atakuwa Martin Saanya kutoka Morogoro na Kamishna ni Emmanuel Kavenga wa Mbeya.

Mgambo Shooting vs African Lyon (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Mwamuzi ni Amon Paul wa Mara wakati Kamishna ni Ally Mkomwa kutoka Pwani), JKT Ruvu vs Mtibwa Sugar (Uwanja wa Azam Chamazi, Dar es Salaam. Mwamuzi ni Israel Mujuni wa Dar es Salaam wakati Kamishna ni Salum Kikwamba kutoka Kilimanjaro).

Tanzania Prisons vs Kagera Sugar (Uwanja wa Sokoine, Mbeya. Mwamuzi ni Ibrahim Kidiwa wa Tanga wakati Kamishna ni John Kiteve kutoka Iringa), Oljoro JKT vs Azam (Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha. Mwamuzi ni Athuman Lazi wa Morogoro wakati Kamishna ni Juma Mgunda kutoka Tanga).

Uwanja wa Jamhuri, mjini Morogoro utatumika kwa mechi kati ya Polisi Morogoro na Coastal Union ya Tanga ambapo Mwamuzi atakuwa Said Ndege wa Dar es Salaam wakati Kamishna ni Hakim Byemba kutoka Dodoma. Toto Africans itacheza na Ruvu Shooting katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ambapo mwamuzi ni Geoffrey Tumaini kutoka Dar es Salaam na Kamishna ni Josephat Magazi wa Singida.

 MECHI ZA MARUDIANO RCL WIKIENDI HII

Mechi za marudiano za raundi ya kwanza ya Ligi ya Mabingwa wa Mikoa (RCL) zinachezwa wikiendi hii katika viwanja kumi tofauti wakati mechi ya Flamingo ya Arusha na Machava FC ya Kilimanjaro yenyewe itachezwa Jumatatu (Mei 20 mwaka huu).

Uamuzi wa mechi hiyo kuchezwa Jumatatu ni kutokana na Uwanja wa Sheikh Kaluta Amri Abeid kutumika kwa mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kesho wakati Jumapili utatumika kwa shughuli nyingine za kijamii kwa mujibu wa wamiliki wa uwanja huo (CCM Mkoa wa Arusha).

 Mechi nyingine zitachezwa keshokutwa (Jumapili) ambapo Abajalo watakuwa wenyeji wa Red Coast kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Dar es Salaam. Uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara utatumika kwa mechi kati ya wenyeji Coast United na Kariakoo ya Lindi.

 African Sports ya Tanga itaoneshana kazi na Techfort ya Ifakara mkoani Morogoro katika mchezo utakaochezwa Uwanja wa Mkwakwani. Nayo Simiyu United ya Simiyu itakuwa mgeni wa Magic Pressure ya Singida kwenye Uwanja wa Namfua, mjini Singida.

 Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza ndiyo utakaotumika kuzikutanisha timu za Polisi Jamii Bunda kutoka Mara na wenyeji UDC wakati Biharamulo FC ya Kagera na Polisi SC ya Geita zitaumana kwenye Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba. 

Milambo FC ya Tabora itakuwa mwenyeji wa Saigon FC ya Kigoma kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora huku Mbinga United ya Ruvuma ikiikaribisha Njombe Mji ya Njombe kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea.

Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini Iringa utatumika kwa mechi kati ya wenyeji 841 KJ dhidi ya Kimondo SC kutoka Mbeya. Nazo Rukwa United na Katavi Warriors zitapimana ubavu kwenye Uwanja wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga.

 Timu zitakazofuzu kucheza raundi ya pili zitacheza mechi zao za kwanza kati ya Mei 25 na 26 mwaka huu wakati mechi za marudiano ni kati ya Juni 1 na 2 mwaka huu.

 UTARATIBU WA SAFARI MECHI YA TAIFA STARS v MOROCCO

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) litasaidia upatikanaji wa visa kwa waandishi wa habari na Watanzania wengine wanaotaka kwenda Morocco kushuhudia mechi kati ya Taifa Stars na Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu jijini Marrakech, Morocco.

Kwa ambao wangependa kupata visa kupitia TFF wanatakiwa kuwasilisha pasipoti zao, ada ya visa ambayo ni dola 50 za Marekani pamoja na picha mbili zenye kivuli (background) ya rangi nyeupe kabla ya saa 6 kamili Mei 20 mwaka huu.

 Boniface Wambura Mgoyo

Ofisa Habari

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

UWT MBEYA WAMJIA JUU MCHUMBA WA DKT SLAA...................

Dkt Slaa akiwa na mchumba  wake Bi Bi.Josephine Mushumbusi Kushoto
......................................................................
Na Esther Macha, Mbeya

UMOJA wa wanawake  wa chama cha Mapinduzi Mkoani Mbeya(UWT) umemshukia Bi.Josephine Mushumbusi ambaye ni mchumba Katibu Mkuu wa chama cha
Demokrasia na maendeleo CHADEMA kufuatia kauli za udhalilishaji dhidiya Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.

Hatua hiyo inatokana  na kauli za kiudhalilishaji zilizotolewa
mwishoni mwa wiki na mchumba huyo wa Katibu Mkuu wa Chadema kuwa mama Kikwete ameshindwa kumshauri   Rais ambaye ni mume wake  kuiongoza nchi vizuri .

Kauli hiyo imetolewa jana na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Mkoa wa
Mbeya Bi.Priscilla Mbwaga wakati  akitoa Tamko   kwa waandishi wa habari juu ya Matusi ya wazi yaliyotolewa na Bi.Mushumbusi   kwa Mke wa Rais katika mikutano ya hadhara iliyofanyika Wilayani Mbozi Kata ya
Vwawa Mkoani hapa.

Bi.Mbwaga alisema kuwa katika mikutano yake ya Hadhara Bi.Mushumbusi alidai kuwa  mama Salma Kikwete  ameshindwa kumshauri  mume wake kuingoza nchi na kuacha Twiga wakiwa wanakunjwa na kuondoka na kwamba yeye akiwa Ikulu hataacha kumshauri mume wake Dkt.Slaa katika masuala
ya kuingoza Nchi.

Hata hivyo Mwenyekiti huyo alisema kama umoja huo wanalaani  vikali lugha chafu na za kichochezi zinazopandikizwa  chuki miongoni mwa jamii ya watanzania .

Alisema kuwa kama umoja wa wanawake  wanalaani matusi hayo na kwamba umoja huo  ulifuatilia  mikutano  hiyo na kugundua kuwa ilikuwa imetawaliwa  na  matusi badala ya kutoa sera  kwa wananchi kuwa wanataka kufanya nini.

“Sisi kama umoja wa wanawake  Mkoa tunaeleza umma  ambao una imani na  kuwa katika utamaduni   na maadili  yao hawapendi  na wala hawajazoea kusikia matusi  katika  jamii yao hivyo wakiangalie vizuri na kwa  makini Chadema  kuwa  cha hicho kina  watu  wa maadili gani , mahali  pote  siku zote  na miaka  yote  ni matusi,kuongea uongo, uzushi  na kashfa wasimamapo majukwaani “alisema Mwenyekiti huyo.

Aidha Bi.Mbwaga alisema kuwa wanawake wa mkoa wa Mbeya  wanadhani kuwa kauli ambazo zimetolewa na  Mushumbusi ni  ni za kuwadhalilisha wanawake wote wa Tanzania  kwani Mama Salma ni Kiongozi wa juu pamoja
na Mushumbusi .

“Tunamshangaa sana  Mushumnbusi anaposimama majukwaani na kutoa kashfa nzito za namna hii ni  kama nani kwa wanawake  wa Tanzania alihoji Mwenyekiti huyo.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Umoja wa vijana wa Chama cha Mapinduzi Mkoani hapa (CCM),Bw.Amani Kajuna  alisema  kauli aliyotoa Dkt.slaa kuwa Rais Kikwete  ana Udini ni ulaghai  mkubwa  ambao anaufanya kwa wananchi  na kuendelea kuiweka nchi katika mazingira magumu .

“Kama vijana  tunatambua kuwa  Rais Kikwete ni kiongozi wa watanzania, na kwamba hana sifa ya Udini hii ajenda inaanzishwa kisiasa ili kujipatia umaarufu wa bure wa kudhani kuwa ndiyo njia ya kuwapeleka ikulu  mwaka 2015 jambo ambalo halitawezekana ,maana  watanzania hawataweza kukubali’alisema Mwenyekiti huyo.

Hata hivyo Bw.Kajuna aliendelea kusema kuwa Dkt. Slaa amekuwa akimtuhumu  Rais Kikwete kuwa  ni FREEMASON , “hebu tumuulize huyu mtu amekutana lini na Rais kwenye iman hiyo” na kwamba katika uongozi wake watanzania  wameona miradi mikubwa  ya maendeleo ya nchi yetu kwa
ukuaji wa wa pato la Taifa.

May 16, 2013

MBUNGE MSIGWA ADAI WANAHABARI 7 MKOANI IRINGA MAISHA YAO YAPO HATARINI ......

 Mbunge Msigwa
 Wanahabari  mkoa  wa Iringa  wakitoka makao  makuu ya  polisi mkoa  wa Iringa siku mwanahabari  wa mtandao  huu alipojisalimisha polisi baada ya  kifo cha Mwangosi kwa madai ya kusakwa na  polisi.
 
 Baadhi ya  wanahabari  mkoa  wa Iringa
 
 Viongozi  wa klabu ya  waandishi  wa habari mkoa wa Iringa katika  picha ya pamoja
...................................
 
Mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji  Peter Msigwa amefichua siri  iliyofichika dhidi ya  wanahabari mkoani Iringa baada ya  kuueleza umma  kuwa zipo njama  zinazopangwa za  kuwaangamiza  wanahabari 7 mkoani Iringa .

Bila  kutaja  majina  ya  wanahabari  hao  wala mhusika na  njama  hizo  za  kuwaangamiza wanahabari hao  Mbunge   huyo alisema  kuwa njama  hizo zinafanywa  kama  njia ya  kuwakomesha  wanahabari ambao  wamekuwa  wakiripoti habari  za mikutano  yake .

Kauli  hiyo ambayo  imepokelewa  kwa  hisia tofauti na  wanahabari mkoani hapa  imetolewa  leo katika mkutano  wake  wa hadhara  uliofanyika katika  eneo la stendi  kuu ya mabasi yaendayo mikoani na  kuwataka  wanahabari  kutorudi  nyuma katika kuandika  ukweli.

" Nawaelezeni  leo  kuwa   wanahabari 7 mkoani  Iringa wapo katika hatari  kubwa na  chanzo  cha  kuwachukia  wanahabari hao ni  kutokana na  kuandika ukweli .....sasa  mimi  nawaombeni  wanahabari  msiogope  fanyeni kazi  yenu  ya  kuhabarisha  umma kwa kuzingatia  maadili na umma utakuwa nyuma  yenu hivi niwaulezeni  leo  hapa vyombo  vya habari  vikiandika na  kutoa picha  hii ya umati mkubwa wa  watu  watakuwa  wamesema  uongo ....sasa  wapo ambao hawataka  kusema mbunge Msigwa atikisa Iringa "

 Katika  hatua  nyingine  mbunge Msigwa alisema  kuwa ataendelea  kusema ukweli hata kama  watamvunja  miguu na  kuwa iwapo  hatakamatwa na polisi kwa  siku  tatu atakazokuwepo  jimboni  Iringa basi atahakikisha  jumapili anawasimamia  Machinga  kufanya  biashara  yao eneo la Mashine  tatu ambalo linazuiwa na  Manispaa ya  Iringa .

Pia  mbunge Msigwa  amelilipua  jeshi la  polisi kwa madai  limekuwa  likiwabambikia watu  kesi  kiasi  cha  njama  hizo  kubainika na hata  mahakama  kuu Tanzania kanada ya  Iringa  kuamua kuliumbua  jeshi  hilo kwa  kukanusha taarifa  yake ya  kudai kumkamata  mlinzi  wa Mahakama kwa kuiba  vielelezo wakati katika mahakama  hiyo hakuna kielelezo aina ya bangi iliyoibwa .





JAJI MKUU WA TANZANIA AELEZA MIKAKATI YA KUBORESHA MAHAKAMA KUU NCHINI .....


Jaji  mku wa Tanzania Mhe.Mohamed Chande
............................................... 
Na Elizabeth Ntambala
Sumbawanga

JAJI mkuu wa Tanzania Mohamed Chande  amesema kuwa mahakama  kuu Tanzania inaendelea na mkakati endelevu wa miaka 2 utakao husisha unoreshajki wa miundombinu ya mahakama za ngazi zote nchini kutoa elimu ya kujiendeleza kwa watumishi wake na pia kuzitolea uamuzi kesi zote zilizochukua mda mrefu.

Jaji mkuu  Mohamed Chande  aliyasema hayo alipokuwa katika ziara yake ya kikazi ya siku ya kwanza ya kukagua maendeleo ya utendaji haki kwa mahakam ya mikoa ya Rukwa na Katavi.

Jaji mkuu wa Tanzania Mh. Mohamed alisema kuwa utekelezaji wa mkakati huo ni moja ya miundombinu za kuondoa usumbufu wanaoupata wananchi wakati wa uendeshaji wa kesi zao na pia kuondoa lawama za muda mrefu za uwajibikaji mdogo na vitendo vya rushwa.

Akiongea na watumishi wa mahakama hizo za hakimu mkazi wilaya na mkoa na baadae watumishi wa mahakama kuu kanda ya sumbawanga alidai kuwa zaidi ya shilingi bilioni 10 zinategemewa ku[itishwa katika mwaka huu wa fedha wa utekelezaji mkakati.

Kwa upande wake hakimu mfawidhi wa mahakama ya wilaya ya Manase Goroba alisema kumekuwepo na changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo hasa ya wapiga chapa ikiwamo ya uchakavu wa majengo mengi ambayo yanahitaji ukarabati mkubwa katika mahakama .

Alisema kuwa kumekuwepo na mahakama mpya ambazo ni zilijengwa kwa nguvu za wananchi na bado majengo hayo hajakamilika hivyo kunahitaji fedha kwa ajili ya umaliziaji wa majengo hayo.
Mustafa sijani ni hakimu wa mwanzo wa wilaya walimweleza jaji mkuu kuwa adha zinazowakabili watumishi wa mahakama katika utendaji wa kazi ni pamoja na uhaba wa watumishi vitendea kazi.

MBUNGE MSIGWA AMKATA KINANA KWENDA MAHAKAMANI KESHO ,PIA AWATAKA MACHINGA KUFANYA KAZI KWA UHURU ZAIDI




Mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini mchungaji Peter Msigwa amewataka  wafanyabiashara  ndogo ndogo (machinga ) mjini Iringa  kuendelea  kufanya kazi katika  eneo la Mashine  tatu  bila  kufanya  vurugu  zozote kwa  wale wanaozuia kufanya  hivyo.

Akizungumzia  suala la Machinga  kuendelea  kunyanyasika  mbunge Msigwa amesema  kuwa tayari suala  hilo ameanza  kulipigania bungeni  kwa waziri  mwenye dhamana  hivyo kamwe  machinga  Iringa  wasikubali  kunyanyasika .

Aidha mbunge  huyo amemtaka  katibu mkuu  wa chama  cha mapinduzi (CCM) Bw  Kinana  kutosubiri muda  wa  siku  21 alizozitoa  kumfikisha mahakamani kuwa  yupo tayari  kwenda mahakamani hata kesho.

Mbunge Msigwa amesema kuwa katika  ukweli kama  hata  kuwa tayari kumwogopa mtu na kuwa siku  zote atasimama katika  ukweli katika  kupigania maslahi ya Taifa  hili.

Mbunge  Msigwa amesema  kuwa hatua ya katibu mkuu  wa CCM kukimbilia katika  vyombo  vya habari  kutishia  kumfikisha mahakamani bila yeye mhusika  kupelekewa taarifa  ni  sawa na kumwogopa na  hivyo suala la Kinana kwenda Mahakamani  si  sawa na  kumtishia nyau mtu mzima.

Kwani  alisema  kuwa  Chadema  ina  mawakili  waliojitosheleza na  kuwa hawatanyamaza kusema  ukweli kwa  kuogopa vitisho vyovyote .
 Mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini akiwahutubia umati mkubwa wa wananchi  wa  jimbo hilo jioni hii katika eneo la stendi kuu ya mabasi ya mikoani



 Umati mkubwa  wa  wananchi  wakimsikiliza mbunge  wao wa  jimbo la Iringa mjini
 Mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini Mchungaji ,Msigwa akiwahutubia  wananchi  wa  jimbo la Iringa mjini

"LIVE" MKUTANO WA MBUNGE MSIGWA WATIKISA IRINGA


 mbunge  wa  jimbo la Iringa mjini  mchungaji Peter Msigwa akihutubia umati mkubwa wa  wananchi katika  eneo la stendi la mkoa  wa Iringa


MAHAKAMA IRINGA YAMGEUKA RPC KAMUHANDA .....................

  kaimu msajili  wa  mahakama kuu Tanzania kanda ya Iringa Godfrey Isaya  akizungunza na  wanahabari leo
 Baadhi ya mahakimu  na  watumishi  wa mahakama  wakimsikiliza kaimu msajili  huyo
 
 Wanahabari  wakimsikiliza kaimu msajili wa mahakama kuu  Tanzania kanda ya Iringa
  kaimu msajili  wa  mahakama kuu Tanzania kanda ya Iringa Godfrey Isaya  akionyesha chumba cha vielelezo ambacho kipo  salama  kabisa
 Hapa  ndipo bangi  hiyo  ilipoteketezwa 
 
 
 
 Dirisha la chumba  hicho  cha  vielelezo mahakamani  likiwa  salama kabisa
..................................................................................................
 
 
 
MAHAKAMA kuu ya Tanzania kanda ya Iringa  imepinga  vikali taarifa  ya  jeshi la polisi mkoa  wa Iringa (RPC) Michael Kamuhanda  aliyoitoa jana kwa vyombo vya habari  kuwa inamshikilia mtumishi  wa mahakama hiyo kwa kuiba bangi iliyofikishwa mahakamani hapo kama kielelezo.
 
"Taarifa  ya kamanda  wa  polisi kuwa bangi  imeibiwa mahakamani si  ya kweli na imelenga  kuichafua mahakama  hiyo na kuwa  wao kama mahakama   hawajapata  kuibiwa na kuwa taarifa  hizo si za kweli kabisa".
 
Akizungumza na  wanahabari  leo ofisini kwake kaimu msajili  wa  mahakama kuu Tanzania kanda ya Iringa Godfrey Isaya alisema  kuwa  wao kama mahakama  wanasikitishwa taarifa  hiyo ya  kuibiwa kwa  vielelezo  iliyotolewa na jeshi la polisi  kuwa haina ukweli  wowote .
 
Isaya  alisema  kuwa jeshi la polisi limepotosha umma kwa kutoa taarifa  ya uogo bila kufanya uchunguzi na  kuwa kama ni kuibiwa  vielelezo ilipaswa  kuwepo kwa mlalamikaji ambaye ni Mahakama kwenda kufungua kesi polisi na si vinginevyo.
 
" Tunakanusha  vikali kuwepo kwa  upotevu  wa kielelezo cha bangi katika mahakama  hii Exhitibit Room haijavunjwa iko intact .....tulikuwa na kielelezo P.3 katika shauri  hilo la jinai namba 24/2012 ambayo ni bangi  viroba 8 amri ya mahakama ya kuteketeza ilitolewa tarehe 13/2/2013 na bangi  hiyo iliteketezwa chini ya uangalizi  wa afisa wa  jeshi la polisi na kesi hiyo  ilikwisha tarehe 13 /2/2013 na mshtakiwa alihukumiwa kifungo cha miaka miwili  jela"
 
Alisema kama ilivyokuwa katika kesi nyingine za jinai tunatoa wito kwa  jeshi la polisi  Iringa kufanya uchunguzi wa kina kuona bangi hiyo imepatikana  wapi kwani  sisi kama mahakama hatujapata kuibiwa bangi katika mazingira  yoyote na kama tukio hili lingekuwepo basi taarifa   polisi zingeripotiwa .
Pia  alisema kama kweli mahakama kuna vielelezo  vilivyoibwa basi polisi  wangefika kufanya upelelezi hata  kuwahoji kama njia ya kuchunguzi .
 
" Tunalishauri jeshi la polisi kufanya utafiti  wa  kina kuhusu  suala hili kabla ya kutoa taarifa katika vyombo vya habari "
 
hatua ya mahakama hiyo kupinga taarifa ya jeshi la polisi mkoa  wa Iringa imekuja siku  moja baada ya  jeshi  hilo kutoa taarifa kwa vyombo vya habari  kuwa  linamshikiria mtumishi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa kwa tuhuma za kuiba vielelezo vya madawa ya kulevya aina ya bangi.

Kwa mujibu  wa kamanda  wa  polisi mkoa  wa Iringa Bw Kamuhanda alisema tukio hilo limefanyika tarehe 14  ambapo mtuhumiwa huyo wa mahakama  Lwitiko Lusekelo Minga ambaye ni mlinzi wa Mahakama ya Wilaya ya Iringa, aliiba bangi yenye uzito wa kg 371.2
“Tukio la kupatikana kwa bangi, eneo la Flerimo mtuhumiwa Juma Nzowa alikamatwa na bangi na baada ya kuhojiwa mtuhumiwa alimtaja Lwitiko Lusekelo Minga Mlinzi wa Mahakama kuwa ndiye aliyemuuzia kielelezo hicho cha mahakama,” Alisema Kamuhanda.
Pia amesema kielelezo hicho awali kilikamatwa Wilaya ya Kilolo na kufikishwa mahakamani kama ushahidi na ndipo ilipoibiwa tena.
Amesema kutokana na uwepo wa watumishi wasio waaminifu kumekuwa na tabia hiyo hasa kwa madawa hayo ya kulevya, vielelezo vyake na kurudi tena mitaani huku wao wakiendelea na zoezi la kukamata.
Hata hivyo kumekuwa na malalamiko mbalimbali juu ya vielelezo hivyo kuibiwa pindi vifikapo Mahakamani, hasa kwa vidhibiti hivyo vya madawa ya kulevya na  vipodozi mbalimbali ambapo huuzwa katika maduka na wananchi kuendelea kutumia.
Aidha vielelezo kama vyombo vya thamani navyo vimesemekana mara nyingi hupotelea Mahakamani na hata katika vituo vya Polisi.
 

 

HUYU NDIE SISTER ' FEKI' RAIA WA KENYA ALIYEKAMATWA KWA UTAPELI IRINGA


 Mwanamke - anayejiita Sister Phylis Wanjiru Kamau, raia wa Kitui nchini Kenya akiwa ofisi za kamanda wa jeshi la Polisi mkoa wa Iringa, baada ya kukamatwa.
Taarifa za kipolisi, za kukamatwa kwa Sister Feki Phylis Wanjiru Kamau.
.....................................................................................

 
MAANDIKO matatatifu ya  kibiblia  yanasema  kuwa siku za mwisho yatatokea mambo mengi ya  kushangaza  dunia ,kamwe kama dalili  za siku  za mwisho basi naweza  kusema ndizo hizi kwani kila kukicha ni mambo mapya ya kushangaza .
 
Wakati Taifa  likiwa katika maswali yasiyo na majibu  juu ya  tukio la bomu kuua Kanisani mkoani Arusha ,mkoani Iringa  mwanamke mmoja anayetambulika kwa Phylis Wanjiru ( 44)raia wa Kitui nchini Kenya amekamatwa akitaka  kuwatapeli Masister wenzake .
 
Mwanamke  huyo akiwa amevalia ya kitawa mfano wa  masister wa kanisa Kathoriki alikamatwa na kufanyiwa upekuzi na kukutwa na baadhi ya vielelezo vilivyothibitisha  utapeli  wake  huo .
 


Wanjiru ambaye ni raia wa nchi ya Kenya amekamatwa na jeshi la polisi baada ya masister wenzie kubaini kama si mmoja wao, kutokana na kushindwa kufanya baadhi ya masuala  ambayo ni msingi wa utawa wao.

Taarifa  kutoka ndani ya jeshi la polisi mkoa wa Iringa zinaeleza  kuwa  mwanamke huyo kabila lake ni Muwembu wa nchini Kenya amekamatwa katika nyumba  za masista zilizopo Ipogolo mjini Iringa.


Hata  hivyo  mwanamke huyo ambaye awali aligoma kutoa maelezo ya kina juu ya ujio wake nchini Tanzania, katika upekuzi walimkuta na baadhi ya chip (Line) za makampuni mbalimbali ya simu ya ndani na nje ya nchi.

 Sister huyo feki alikutwa pia akiwa na hati za kusafiria (Passport) mbili, moja ikiwa niya Africa Mashariki yenye namba Ke. 020659 huku hati ya nyingine ikiwa na jumuiya ya Kenya namba A. 1790366.


Amesema Sister huyo feki katika hati hizo ilionyesha kuwa alitembelea nchi ya Rwanda, Uganda pamoja na nchini Tanzania ambapo siku za hivi karibuni alikuwa Mkoani Mara Tarime.
Sister huyo amekuwa akitumia mbinu ya kujiangusha kama mtu mwenye ugonjwa wa kifafa pindi anapofanyiwa mahojiano, jambo linalowawia vigumu jeshi hilo kupata maelezo ya kina dhidi ya dhamira yake ya kuingia humu nchini.

May 15, 2013

WANANCHI TARAFA YA ISIMANI WAMPONGEZA MBUNGE LUKUVI KWA UMEME NA BARABARA YA LAMI

 

Tanesco wakiendelea  kusambaza  umeme  Tarafa ya  Isimani  jimboni kwa waziri Lukuvi
 
...................................................................................................
 
WANANCHI  wa  tarafa  ya  Isimani jimbo la Isimani  wilaya ya  Iringa  vijijini  mkoani  Iringa  wamempongeza  mbunge  wa  jimbo la Isimani Bw. Wiliam Lukuvi kwa  kuwapigania kupata  umeme  wa gridi ya  Taifa  na ujenzi  wa barabara  ya lami  ya Iringa- Dodoma.

Wananchi hao  wametoa  pongezi  hizo   leo katika  ukumbi  wa Hima  wakati  wa  semina ya  siku  moja ya mradi  mpya  wa  kuwasaidia kuwakopesha  n'gombe  kupitia mradi  wa  kopa ng'ombe  lipa ng'ombe  mradi unaofadhiliwa  na asasi  ya  Heifer (HPI) 

Kwani  wamesema  kuwa  mbali ya  tarafa  hiyo ya  Isimani na  wilaya  nzima ya  Iringa vijijini katika  Historia ndio  ilikuwa ni  wilaya  pekee  iliyoweza  kulisha  mkoa wa Iringa kutokana na kuongoza katika uzalishaji  wa mazao  ya chakula  ila kwa  sasa uzalishaji huo  umebaki  kuwa  historia  baada ya  eneo hilo  kuathiriwa  zaidi na mabadiliko tabia nchi .

Hivyo   walisema maisha yao  kwa  sasa  wamekuwa  wakitegemea  jitihada mbali mbali ambazo  zimeendelea  kufanywa na mbunge  wao  huyo kutokana na kuendelea  kuwapigania  kwa  kuanzishwa kwa miradi mbali mbali  ukiwemo mradi mkubwa wa umeme ,barabara  ya lami na  sasa  mradi  wa maji ambao utatatua kero ya maji katika tarafa  hiyo ya Isimani.

Wananchi hao  walisema  kuwa  moja kati ya  changamoto  kubwa  zinazowakumba ni  pamoja na  kukosekana kwa huduma ya maji  katika  eneo  hilo kutokana na ukame  unaokabili  eneo  hilo ila kwa  sasa  suala  hilo  limekuwa  likishughulikiwa na  mbunge  wao Lukuvi. 

Bw Felix Sanga  alisema  kuwa Kuhusu tatizo la ukame  unaoendelea  kuwakumba katika tarafa    kuwa  suala  hilo  lina ufumbuzi  wake  ikiwa ni pamoja na  kujipanga kwa  utunzaji  wa mazingira  kwa  wao  wenyewe  kuweka utaratibu  wa  kutunza mazingira yanayowazunguka. 

Kuhusu  ujenzi  wa  barabara  ya lami kati ya Iringa- Dodoma  unaoendelea  Sanga alisema  kuwa  mradi huo  wa barabara  utaweza  kufungua mirango ya  kiuchumi kwa  wananchi  wa tarafa  hiyo ya Isimani na  kupongeza jitihada za mbunge na jinsi anavyoendelea  kupigania maendeleo ya  wananchi wake. 
 
 Kwa  upande  wake  mtaalam  kutoka  asasi  hiyo ya  Kimataifa ya Heifer   Interinational  Dr Emmanuel Sokonde  alisema   kuwa lengo la mafunzo  hayo ni maandalizi ya  kuandika andika  maalum kwa ajili ya  kushawishi asasi  hiyo  kusaidia miradi ya  kiuchumi  ukiwemo mradi  wa ufugaji  wa ng'ombe. 

Hivyo  alisema  kuwa  lengo la  asasi hiyo ni kuwakomboa  watanzania  na kuwatafutia miradi yenye  kuwakwamua  kiuchumi  zaidi na  kuwa iwapo  watafanikiwa  mradi huo  kufika  eneo hilo basi itakuwa ni faida kwa  wananchi wa tarafa  hiyo.

KAMPUNI YA UCHIMBAJI WA VISIMA YATUA IRINGA KWA HUDUMA ZAIDI

BUSIGER DRILLING COMPANY ni jibu lako sasa kwa huduma ya uchimbaji visiwa nchini Tanzania
Iwapo wewe ni taasisi ,kampuni ama mtu binafsi wahitaji kumiliki kisima cha maji cha kisasa kwa gharama nafuu zaidi ,usipate shida sasa
Ni wachimbaji maarufu wa visiwa vya kisasa kwa gharama nafuu zaidi
Wasiliana nasi kwa namba 0774100 100 tutakufikia popote ulipo ndani ya Tanzania

WANYWAJI WA VIROBA DAR WAPINGA VIROBA KUPIGWA MARUFUKU

Wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Viwanda na Biashara, wakiangalia uzalishaji walipotembelea kiwanda cha Konyagi cha Tanzania Distilleries Limited (TDL), Dar es Salaam hivi karibuni.

 ...............................................................................................
Na Mwandishi Wetu.

BAADHI ya wananchi jijini Dar es Salaam, wamelalamikia hoja iliyozuka bungeni wiki hii kwamba kinywaji cha Konyagi aina ya Kiroba kipigwe marufuku nchini.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi hao, walisema endapo serikali itachukua uamuzi wa kupiga marufuku kinywaji hicho, watarudia kunywa pombe aina ya gongo ambayo ni hatari kwa afya zao.

Mkazi wa Mbagala, Faustine Mwiruka aliyekutwa kwenye baa ya Kisuma, aliiasa Serikali kutothubutu kukubali kinywaji hicho kupigwa marufuku, kwani ikifanya hivyo wengi wa wananchi wenye kipato cha chini wataanza tena kunywa gongo na pombe za kienyeji.

Itabidi tufanye kama Zambia ambao wamezuia viroba, lakini nchi nzima imejaa viroba vya Malawi, Zaire na Burundi, lazima tuiadhibu serikali ikose kodi kote kote, bia hatunywi, viroba vya nje tutakunywa, pamoja na gongo.


Alisema haingii akilini kukihusisha kinywaji hicho na ajali za magari, akidai kuwa hata kabla ya viroba kuingia sokoni ajali zilikuwepo nyingi.

"Sisi tuna imani na viroba kwa vile vina ubora wa uhakika tofauti na pombe ya gongo ambayo inapikwa bila kupimwa ubora hivyo ni hatari kwa usalama wa afya zetu." alisema Mwiruka.

Naye Ali Hassan mkazi wa Kinondoni kwa Manyanya, alisema, wanaotaka viroba vipigwe marufuku hawawatendei haki wananchi wa kawaida ambao kwa asilimia kubwa hawana uwezo wa kununua bia ambazo bei yake ni kubwa.

Mwandishi wetu aliyetembelea maeneo ya Ilala Kota Mchikichini alifanikiwakuhojiana na wakazi wa eneo hilo ambao wengi wao walisema kuwa jambo hilo lililozushwa wiki iliyopita wanaamini ni njama za wafanya biashara toka nchi jirani ambao hawaitakii mema Tanzania kwa kuwa pombe hiyo kuwepo kwake pia kunakuza pato la Taifa.

Juma Pingu alisema kuwa haoni sababu ya kupiga marufuku viroba kwakuwa ni pombe ya wanyonge na kuwataka wabunge kuthamini bidhaa za nyumbani kwanza.

Akizungumza na waandishi wa habari mwanzoni mwa wiki hii, Mkurungenzi Mkuu wa Konyagi, David Mgwassa alisema kuwa kwa kipindi kirefu kumekuwa na mchezo mchafu wa kuharibiana jina sokoni kwa kutumia baadhi ya vyombo vya habari vya hapa nchini, kampeni inayoendeshwa na makampuni yenye uhusiano na makampuni makubwa ya pombe duniani yasiyo penda, nchi za afrika zizalishe pombe zake, bali ziendeleee kununua kutoka Ireland, wales. Kenya and uingereza.

Wadau hao wa Pombe nchini walifikia uamuzi wa kutoa maoni hayo baada ya kuona kuwa kinywaji chao Kiroba kinapigwa vita lukuki kwenye magazeti. Huwezi ukahusisha viroba na piki piki, kwani nchi hii ina piki piki laki tatu, na wananchi million 43, uhusiano wake uko wapi, kwanza hata leseni hamuwapi?

May 14, 2013

KUFUATIA MGOMO WA DALADALA IRINGA , SUMATRA YAKUNJUA MAKUCHA SASA YATISHIA KUWATIMUA KAZI MAOFISA WAKE .......

 Mmiliki  wa daladala akiwasilisha kero  yake kwa uongozi wa Sumatra
 Mmoja kati ya madereva hao na mmiliki wa daladala Bw Peter akitoa maoni yake kwa Sumatra.
 Baadhi ya madereva wakitoa maoni yao juu ya kero  wanazozipata
SAKATA  la  mgomo  wa  daladala katika Manispaa ya  Iringa limeanza  kushughulikiwa kwa kasi kubwa na mamlaka ya uthibiti ,usafiri  wa majini na nchi kavu (SUMATRA) makao makuu  baada ya  kutuma maofisa  wake  kutoa elimu kwa wamiliki  huku mamlaka  hiyo ikiapa kuendelea  kupambana madereva wanaonyanyasa abiria kwa kuvunja  wa  sharia.

Pia  imeapa  kuwachukulia hatua kali  ikiwa ni pamoja na kuwafukuza kazi maofisa  wake ambao  watabainika kupokea faini ndogo kinyume na faini  inayopaswa  kulipwa kisheria.
Akizungumza na  wamiliki  wa daladala na madereva leo  katika  ukumbi wa shule ya  Sekondari Lugalo ,  kaimu mkurugenzi wa idara ya usafiri  wa barabarani Bw Leo Ngowi alisema  kuwa ni  vema wamiliki  wa daladala na  madereva kuheshimu  sharia za usafirishaji ikiwa ni pamoja na  kuzitambua sharia  hizo pia  wasiwe nyume  kuwafichua maofisa wanaukula  rushwa .
Ngowi  alisema  kimsingi katika  sharia  za Sumatra  kuna faini  za aina mbili  ikiwemo ya Tsh 500,000 ambapo nusu yake Tsh 250,000 na  faini  nyingine ni Tsh 100,000 na nusu yake ni Tsh 50,000 na  kuwa hakuna faini ya chini ya hapo na iwapo kuna mtendaji anapokea  chini ya viwango  hivyo atafukuzwa kazi mara  moja. 

Pia Alisema kuwa  mamlaka  inapiga   marufuku kwa madereva wa  vyombo  vya usafiri  kupakia wanyama kama mbuzi ,ama mkaa pamoja  na  vitu  vingine  vya  hatari  kwa abiria .

Pamoja na kuapa kuendelea  kusimamia sharia  bado SUMATRA  afisa  huyo alisema   kuwa  utendaji kazi  wake ni masaa 24 hivyo  madereva  wasifikiri kuwa mamlaka  hiyo ina muda  wa  maalum wa kufanya kazi .

 Alisema  kuwa  sheria  hizo  zimewekwa  ili  kuhakikisha kuwa  sekta  hiyo ya usafiri inaboreshwa na  kusiwepo  kwa malalamiko  kutoka pande mbili ya mtoa huduma na mpokeaji wa  huduma  husika.

" Sheria  zinzohusu sekta  ya  usafirishaji ni pamoja na  sharia  ya  viwango ya  mwaka 1975,sheria namba 30 ya  mwaka 1973 ya  usalama barabarani  sharia  namba  1 ya 1973 ya leseni za usafirishaji  na  sharia nyingine nyigi ambazo wanapaswa  kuzitambua"

Hata  hivyo  alisema  kuwa  kwa mujibu  wa sharia  za Sumatra  haziruhusu  kwa daladala  moja ama chombo kimoja cha usafiri  kumiliki  leseni mbili  za njia na kuwa iwapo wapo  wanaofanya hivyo ni kinyume.
Ngowi alisema  kuwa  kitendo  cha daladala  kushusha abiria  njiani hata kama ni abiria mmoja ni kosa na kuwa lengo la usafiri  wa daladala ni kushusha na kupakia na  kuwa kwa kawaida  usafiri  wa mijini huwa haukai sehemu  moja kama ilivyo mabasi ya vijijini ambayo yamekuwa yakiegesha sehemu moja kugonja abiria.

"Hakuna  sharia  inayoruhusu usafiri  wa mjini kukaa sehemu  moja kwa  zaidi ya dakika  20 na  kuwa kwa kawaida  usafiri  wa mjini ni kushusha na kupakia na kuendelea na safari ...,kama  kituo kimoja hakina abiria  basi kituo kinachofuata  kitakuwa na abiria na hata kama kuna abiria wawili ama mmoja haki yake ya msingi kufikishwa hadi mwisho wa safari kwa mujibu wa leseni ya  njia"

Aidha  alisema  kuwa Sumatra imesitisha  utoaji  wa leseni kwa magari  yenye  uwezo  wa  kubeba abiria  kuanzia  7 hadi 12 iwapo yatatumika kwa matumizi binafsi na namba  za usajili ni zile za njano si  vinginevyo .

Ngowi  alisema  kuwa upande wa madereva ni lazima  kabla ya kuanza kazi kumfahamu vema mmiliki wa gari analoliendesha ikiwa ni pamoja na anuani na namba  za simu .

Pia  aliwataka madereva  kukataa kuendesha gari iwapo litabainika  kuwa ni linaloweza kuhatarisha usalama  wake na abiria  wake .

Hata  hivyo alisema  kuwa ni  wajibu kwa mmiliki wa gari  kumtafutia abiria wake chakula  iwapo gari  hilo  litaharibika kwa zaidi ya masaa mawili na kuendelea  ama sehemu ya kulala  iwapo gari  hilo halitaendelea na  safari na sharia  hiyo kwa magari yanayofanya  safari ndefu  kwa  maana ya mikoa.

Wakati  kwa  upande  wa  daladala  ni marufuku  kusimama kituoni kwa zaidi ya dakika 5 katika  kituo  kimoja na kufanya  hivyo ni kosa  kisheria.

Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji  wa Halmashauri ya Manispaa ya Iringa Terresia Mahongo alisema  kuwa  lazima  Sumatra  kuweka mkakati  wa kuwasaidia wananchi ambao  wameendelea  kupata kero  kubwa ya  usafiri kwa madereva  wa daladala kuwakalisha  abiria kwa muda mwingi eneo la posta .

Kuhusu suala la kukosekana kwa choo katika eneo la Isakalilo alisema  kuwa anawahakikishia madereva hao kuwa lazima kero  hiyo ataifanyia kazi ikiwa ni pamoja na kujenga  choo mapema  zaidi  eneo hilo . 

Wakati madereva  hao  walilalamikia  suala la ubovu  wa barabara  kuwa  baadhi ya njia kama ya Mikimbizi  daladala  zimekuwa  zikikwepa  kwenda huko kutokana na njia  hiyo kuwa na mawe mengi na njia kuwa mbovu kupita kiasi hivyo wanataka suala la njia  kurekebishwa  zaidi.

Huku mkurugenzi  wa Manispaa ya  Iringa akiahidi kutengeneza barabara  hizo ndani ya wiki mbili zijazo ili kuwa na barabara  nzuri  zaidi.

Wakati  huo  huo mkurugenzi wa Manispaa ya Iringa Bi.Mahongo amekataa ombi la madereva na  wamiliki wa daladala mjini Iringa la kutaka kikao kijacho  kati ya wadau wa usafiri na madereva na Manispaa kukutana majira ya saa 2 usiku na kuwa kwa muda  huo hawapo tayari kufanya  hivyo.
" Mnataka  tukutane usiku  ili iweje pia na mimi ni kiongozi wa umma ninalindwa na sharia  za utumishi  wa umma sasa mkisema tukutane usiku sitakuwa tayari labdala iwe saa 10 jioni kama ambavyo baadhi yenu mmependekeza iwe saa 10 jioni siku ya jumapili nipo tayari "
Hivyo alisema kikao hicho kitakuwa cha wamiliki pekee wa daladala na si vinginevyo huku akidai kuwa lazima  chama cha madereva wa daladala mjini Iringa kuchunguzwa upya kwani ndicho chanzo cha yote haya.

HYPERLINK SCHOOLS OF TANZANIA SASA IMEHAMIA ENEO LA MLANDEGE MWISHO WA LAMI


Shule  hii  ipo barabarani kabisa Mlandege mwisho  wa lami upande wa kulia kama unaelekea Kidamali na mkono  wa kushoto kama unatoka  Kidamali    

Awali ilikuwa na matawi Kihesa, Ipogolo na Mlandege kama inavyoonyesha hapa juu katika tangazo hilo   ila sasa ni Mlandege mwisho wa lami pekee   
......................................................................................................    

Kumbuka  iwapo  unahitaji  mtoto wako  kupata  elimu  bora  zaidi yenye kumjenga kimaisha  zaidi ,mlete  mwanao hapa  ili apate elimu  yenye kumwezesha  kuja  kuwa kiongozi ama msomi mwenye  kulikomboa Taifa .
 
Tunapokea  watoto  kuanzia  kutoka pande zote za mji wa Iringa usafiri  hadi nyumbani kwako ,pia  huduma ya  chakula na uji ipo ada  zetu ni zaidi ya  bure .
 
Piga  simu    0767 030406

HABARI NJEMA KWA WAKAZI WA MKOA WA IRINGA , ILE KAMPUNI MAARUFU YA UCHIMBAJI VISIMA VYA KISASA SASA NDANI YA IRINGA


BUSIGER DRILLING COMPANY   ni  jibu lako  sasa  kwa  huduma ya uchimbaji  visiwa nchini Tanzania
 Iwapo  wewe ni taasisi ,kampuni ama mtu  binafsi wahitaji kumiliki  kisima cha maji cha kisasa kwa  gharama nafuu  zaidi ,usipate  shida  sasa
 Ni  wachimbaji maarufu  wa visiwa vya  kisasa kwa  gharama nafuu  zaidi
Wasiliana nasi kwa namba 0774100 100 tutakufikia  popote  ulipo ndani ya Tanzania
 
Usipate  shida  kampuni hii imetua mjini Iringa kwa  zaidi ya  wiki  mbili  itaendelea  kutoa huduma ya  kuchimba visima virefu kwa gharama poa  kabisa , waweza wapigia  simu ama fika kituo  cha  Mafuta  ya Hope Service Station jirani na banki ya  CRDB