June 19, 2013

MNYIKA KUONGOZA KUAGA MIILI YAWALIOKUFA KWA MLIPUKO WA MABOMU ARUSHA KESHO

  Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe aliyevaa nguo nyeusi pamoja na Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema aliyevaa skafu shingoni wakiwa nyumbani kwa wazazi wa mmoja wa marehemu (Ramadhani) eneo la Mianzini kuwapa pole kwa kuondokewa na mpendwa wao,katika shambulio la kigaini jijini Arusha juzi.            Pamela Mollel,Arusha 
WAKATI Jeshi la Polisi Mkoani Arusha ikiendelea kumsaka Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini Godbless Lema,Mbunge wa Ubungo John Mnyika kesho atawasha moto mwingine wa maombolezo uliotawanywa kwa mabomu jana.

Mnyika atakuwa msatari wa mbele kuongoza wafuasi wa Chadema kuaga miili ya watu watatu waliouawa katika shambulio la kigaidi Jumamosi iliyopita kwenye Uwanja wa Soweto.

Mbali na Mnyika zoezi hilo pia litasimamiwa na wabunge wanne wa Chadema walioachiwa huru kwa dhamana leo kwakua upelelezi wa kesi zao hazijakamilika.

 wabunge hao , waliachiwa huru kwa dhamana katika Kituo Kikuu cha Polisi Mkoani hapo kabla ya kufikishwa Mahakamani na kutakiwa kurudi Polisi Julai 22 mwaka huu .

Wabunge hao Said Arfi (Mpanda Mjini), Tundu Lissu (Singida Mashariki), Mustapha Akunaay (Mbulu) na Joyce Mukya (Viti Maalumu), walipewa dhama hiyo majira ya saa nane mchana.
Kabla ya Wabunge hao kuachiwa  kwa dhamana, maelfu ya wafuasi wa Chama hicho walijazana katika Mahakama hiyo wakisubiri msafara wa wabunge hao, na mara baada ya kupewa taarifa kwamba wabunge hao wameachiwa huru wakiwa  Polisi,maandamano makubwa yakaelekea katika Kituo cha Polisi.

 Akizungumza baada ya dhamana hiyo Tundu Lissu alisema kwamba, Jeshi la Polisi limempa hasara kubwa baada ya kuvunja mawani yake na kwamba hivi sasa hawezi kufanya kazi yoyote mpaka atakapo pata mawani mapya.

Mbunge wa Ubungo John Mnyika aliyefika jijini Arusha kwa ajili ya kuwawekea dhama wabunge hao alisema kwamba, Chama hicho bado kitaendelea na mipango yake ya kuomboleza na kutoa heshima za mwisho kwa marehemu waliouawa kwa shambulio la bomu katika mkutano wa kisiasa wa Chama hicho Juni 15 mwaka huu katika Uwanja wa Soweto, marehemu hao  ni pamoja na Judith Moshi, Ramadhan Juma na Amir Ally, waliofariki kwenye mlipuko wa bomu.

Akizungumza na waandishi wa Habari baada ya kutoka Polisi Mnyika alisema, "Kesho tutaendelea na zoezi la kuwaaga wenzetu waliofariki dunia katika mkutano wetu, na watazikwa kwa heshima zote za Chama,zoezi litaanzia kanisani kabla ya kwenda katika eneo maalum ilipoandaliwa kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho". Hata hivyo Mnyika alikataa kujata jina la kanisa muda wala eneo iliyopangwa kwa madai kwamba ni mapema sana.

KARIBU RAIS OBAMA TANZANIA

Hili  ndilo  jiji la Dar es Salaam lin linavyoonekana usiku  wa  leo ukiwa eneo la posta mpya
Rais  Jakaya  Kikwete akisalimiana na Rais wa Marekani Barack Obama
Jiji  la Dar es Salaam  linavyopendeza  leo
 

Kama  ilivyoada ziara  za  Rais  wetu mpendwa Dkt Jakaya  Kikwete  zimekuwa na mafanikio nje ya Tanzania hivyo ni matumaini  yetu ujio  wa Rais  Obama nchini ni sehemu ya mafanikio  yetu ,hivyo  watanzania   tunapaswa  kufunika itikadi zetu  za vyma  na kuungana  kuupokea ugeni  huu mkubwa na asiwepo mtu mwenye  kutia doa nchi  yetu KWA UDHAMINI WA SHABIBY BUS LINE  NI USAFIRI  WA  UHAKIKA NA  SALAMA KABISA NA  HOPE SERVICE STATION IRINGA



Abiria  wakiwa  ndani ya basi la Shabiby Line ambalo ni  Full Luxury lenye  choo ndani na  huduma  nyingine  zote ndani

HOPE SERVICE STATION HAPA HUDUMA NI MASAA 24

 Wengi  hukimbilia  kununua mafuta hapa HOPE SERVICE STATION eneo la CRDB barabara ya Iringa -Dodoma katikati ya mji  wa Iringa  kituo  kinachouza mafuta masaa 24 ,wewe wasumbuka na nini  jiunge  na kituo  cha  wengi  sasa .

MRISHO MPOTO NA MJOMBA BAND KUHAMASISHA KAMPENI YA KUNAWA MIKONO NA USAFI WA MAZINGIRA KATIKA MIKOA MITANO NCHINI


IMG_1058  
Msanii wa kughani na kuimba nyimbo za asili Mrisho Mpoto ambaye pia ni Mkurugenzi wa ‘Mjomba Band’ akizungumza na Mhariri wa Mo Blog Lemmy Hipolite (kushoto) kuhusiana na kampeni ya kunawa mikono kwa sabuni na ujenzi wa vyoo bora ili kuepukana na maradhi yanayosababishwa na uchafu. Kampeni hiyo itafanyika katika mikoa mitano hapa nchini ikianzia na Dodoma, Mara, Njombe. Rukwa na Tanga.
Mwanamuziki na mghani maarufu wa nyimbo za asili ya nyumbani Mrisho Mpoto amewataka wasanii na wanamuziki wote nchini Tanzania kuwa kitu kimoja kwa kujenga ushirikiano na muungano ili kuweza kuufikisha muziki wa hapa nyumbani katika malengo ya kimataifa.

Akizungumza na Mtandao Maarufu wa Habari jijini Dar es Salaam, Msanii huyo Mrisho Mpoto maarufu kama ‘Mjomba’ amesema katika kujulikana kwenye michezo kama inayofanyika kwa sasa, vikundi vya uhamasishaji vinavyotumia sanaa ya asili ni muhimu kutumika ili kuweza kukuza lugha pamoja na utamaduni wa nyumbani.

Amesema ili kufanikisha usafi wa mazingira ikiwemo siku ya kimataifa ya kunawa mikono ni muhimu jamii ya watanzania kuzingatia usafi ili kuepukana na magonjwa ya kuambukiza yanayotokana na uchafu unaoambukiza maradhi yanayotokana na uchafu.

Aidha amesisitiza jamii kujenga utamaduni wa kujenga na kutumia vyoo bora na kuboresha mzingira kwa ujumla ili kuhakikisha elimu hiyo inawafikia walengwa kwa kubadili tabia na njia mbadala za mawasiliano kuhusu elimu hiyo.

Amesema mwaka 2010 aslimia 9 tu ya wananchi waishio vijijini na asilimia 22 ya wananchi waishio mijini waliweza kupata huduma bora za usafi wa mazingira.

Katika kampeni hiyo Mrisho Mpoto na kundi lake la Mjomba Band wataanzia mikoa ya Dodoma, Mara, Njombe, Rukwa na Tanga kabla ya kuendelea mikoa mingine ambayo kwa pamoja na watashirikianana na Wizara ya Afya na Ustawi wa jamii.

MAHAKAMA YA RUFAA YAITISHA MADAJALA YA LWAKATARE

Mahakama ya Rufaa imeagiza  kupelekwa majalada yote ya kesi inayomkabili Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Wilfred Lwakatare na mwenzake Lodvick Joseph.
 
Washitakiwa hao wanakabiliwa na shitaka la kula njama kutaka kumnywesha sumu Mhariri wa Gazeti la Mwananchi, Dennis Msacky.
 
Kwa Mujibu wa Msajili wa Mahakama Kuu, Projest Kahyoza, amepokea amri ya Mahakama ya Rufani kuitisha jalada la Lwakatare lililopo Mahakama Kuu pamoja na Kisutu na kuunganishwa kwa pamoja na kupelekwa mahakamani hapo.
 
Hatua hiyo imefuatia Mkurugenzi wa Mashitaka nchini (DPP) kuwasilisha ombi la marejeo ya kutaka kuitishwa majalada ya kesi hiyo ili kuona uhalali wa uamuzi wa Mahakama Kuu wa kumfutia mashitaka ya ugaidi Lwakatare. 
 
Machi 8, mwaka huu, Lwakatare na mwenzake walipandishwa kizimbani mahakamani hapo na kusomewa mashitaka manne likiwemo la ugaidi.
 
Hata hivyo, Mei 8, mwaka huu, Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ilimfutia Lwakatare mashtaka matatu ya ugaidi yaliyokuwa yanamkabili na kubakiwa na shitaka moja la kula njama kumnywesha sumu Msacky.
 
Uamuzi huo ulitolewa na Jaji wa Mahakama hiyo, Lawlance Kaduri baada ya kupitia maombi yaliyowasilishwa na  Mawakili wa Lwakatare na kusema kuwa DPP hakuwa na uhalali wa kufuta kesi ya awali iliyofunguliwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Machi 18, mwaka huu na muda mfupi kuirudisha mahakamani hapo kwa hakimu mwingine.

MTANDAO HUU UNAUNGANA NA WATANZANIA WOTE WAPENDA AMANI NA UTULIVU KUMKARIBISHA RAIS BARACK OBAMA NCHINI

Rais  Jakaya  Kikwete akisalimiana na Rais wa Marekani Barack Obama
Jiji  la Dar es Salaam  linavyopendeza  leo
 

Kama  ilivyoada ziara  za  Rais  wetu mpendwa Dkt Jakaya  Kikwete  zimekuwa na mafanikio nje ya Tanzania hivyo ni matumaini  yetu ujio  wa Rais  Obama nchini ni sehemu ya mafanikio  yetu ,hivyo  watanzania   tunapaswa  kufunika itikadi zetu  za vyma  na kuungana  kuupokea ugeni  huu mkubwa na asiwepo mtu mwenye  kutia doa nchi  yetu KWA UDHAMINI WA SHABIBY BUS LINE  NI USAFIRI  WA  UHAKIKA NA  SALAMA KABISA NA  HOPE SERVICE STATION IRINGA



Abiria  wakiwa  ndani ya basi la Shabiby Line ambalo ni  Full Luxury lenye  choo ndani na  huduma  nyingine  zote ndani

HOPE SERVICE STATION HAPA HUDUMA NI MASAA 24

 Wengi  hukimbilia  kununua mafuta hapa HOPE SERVICE STATION eneo la CRDB barabara ya Iringa -Dodoma katikati ya mji  wa Iringa  kituo  kinachouza mafuta masaa 24 ,wewe wasumbuka na nini  jiunge  na kituo  cha  wengi  sasa .



WATUMISHI WA AFYA RUKWA WATAKIWA KUTANGULIZA UZALENDO


 Na Elizabeth Ntambala
    Rukwa

IMEELEZWA kuwa uzembe unaofanywa na baadhi ya watumishi katika idala ya afya,wizi na kutotolewa takwimu sahihi za afya  kwenye vituo vyao kunakofanywa na halmashauri ya wilaya ya kalambo mkoani Rukwa kumekuwa kukipunguza imani kwa wananchi kwa serikali yao kutokana na kukosa huduma bora za tiba

Hayo yamebainishwa wadau mbalimbali wa  sekta hiyo ya afya katika halmashauri hiyo katika kikao cha kazi na tathimini ya utendaji wao kilichofanyika mji mdogo wa matai,ambapo baadhi ya watumishi walitajwa kuwa ni tatizo katika utoaji wa huduma za tiba kwa kuendeleza mambo hayo sanjari na rushwa kwenye vituo vyao.

Pia kikao hicho kilianza kwa kutoa taarifa ya mganga mkuu wa wilaya hiyo ya kalambo Hosea Mangombe ambapo aliuomba uongozi wa halmashauri hiyo kutowafumbia macho watumishi wazembe ili mikakati yao ya upatikanaji wa huduma baora za tiba katika wilaya hiyo mpya iweze kufanikiwa

Kwa upande waka mwenyekiti wa halmashauri hiyo Godfrey Sichone alisema kilio kikubwa kipo kwa wakina mama wajawazito wanaosumbuliwa kwenye zahanati na vituo vya afya.

Akifungua mkutano huo mkuu wa  wilaya Kalambo moshi Changa aliwataka watumishi hao kuzingatia sheria zao za utumishi kwanza ndipo wadai haki zao.

mwisho.

VOTE FOR TANZANIA REPRESENTATIVE "NANDO" IN THE BIG BROTHER AFRICA 8 THE CHASE



Our Tanzania representative for 2013 Big Brother Africa 8 The Chase
"Nando"  is up for eviction this weekend

To save him from being evicted please do vote for him:

*      Sms - name Nando to 15456


*      Website go to
www.bigbrotherafrica.com<http://www.bigbrotherafrica.com> and login in
your details. Then select VOTE & WIN icon which will give you names of
nominated housemates.

Click on the one you would like to vote for....vote for Nando.

Please note you can only vote on the website once every hour, please
do vote as many time as possible.

Tanzania we can do it.....

Let us encourage our Friends, neighbors and family to vote and save
our fellow Tanzanian from other country using below short code

Vote "Nando" to below short code

Country

Short Code

Kenya

22626

Uganda

7626

Nigeria

34350

South Africa

34624

Zambia

414

Malawi

15626

Sierraleone

2626

Zimbabwe

33334

Namibia

15626

Ghana

1474

Botswana

16626

Angola

44555

Ethiopia

8089

Rest Of Africa

(+)2783142100414

MARUFUKU KAMPENI UCHAGUZI MDOGO WA UDIWANI ARUSHA -NEC

 
 Msajili  wa  vyama vya  Siasa Bw.John Tendwa
..................................................................................................................
Tume ya Taifa ya Uchaguzi-NEC, imevikataza vyama vya siasa vinavyoshiriki katika Uchaguzi Mdogo wa Madiwani kwenye Kata Nne za Arusha Mjini, kutofanya kampeni katika kipindi hiki ambacho uchaguzi huo umehairishwa hadi Juni 30 mwaka huu.
 
                   Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume hiyo, JULIUS MALLABA amesema kwamba Sheria za uchaguzi haziruhusu kwa sasa vyama vya siasa kufanya Kampeni kwa kuwa uchaguzi katika Kata hizo umeahirishwa na kwamba muda wa Kampeni ulikwisha.
                   Vyama ambavyo vitaonekana kukiuka taratibu hizo zitachukuliwa hatua na Kamati za Maadili ambazo zinajumuisha wajumbe kutoka vyama vyote vya siasa nchini.
          MALLABA pia ametoa wito kwa wananchi wa Kata hizo Nne za Themi, Kaloleni, Kimandolu na Elerai ifikapo siku ya kupiga kura, washiriki zoezi hilo kwa Amani na Utulivu.
          Katika hatua nyingine, Mkurugenzi wa Operesheni na Mafunzo, Kamishna PAUL CHAGONJA ameendelea kumsisitiza Mwenyekiti wa CHADEMA, FREEMAN MBOWE kama kweli anao ushahidi wa mtu aliyerusha Bomu auwasilishe kwa Jeshi hilo.
          Amesema hatua hiyo italisaidia Jeshi hilo katika uchunguzi wake ambapo hadi sasa watu Watatu wanashikiliwa na Jeshi hilo kwa mahojiano.
          Pia Kamishna CHAGONJA amekanusha taarifa zinazodai Eti mtu aliyerusha Bomu hilo ni Polisi na ametaka mwenye ushahidi huo aupeleke ili kurahisisha Uchunguzi.

ZIARA ZA RAIS KIKWETE ZALETA FAIDA KWA TAIFA KISOKA , SASA ACADEMY YA MPIRA WA MIGUU KUJENGWA NCHINI ASEMA WAZIRI MUKANDARA

 Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukandara akinzungumza na  wanahabari  mchana  juu  jijini Dar es Salaam ofisini  kwake 
 Wanahabari  wakimsikiliza  waziri Mukandara


 Mpiga picha mkuu  wa Jambo  leo na kamanda wa matukio Richard Mwaikenda kulia akitafakari  swali na  kumuuliza  waziri
.............................................................................................
Mpigapiga  mkuu  wa gazeti la Jambo leo Richard Mwaikenda kulia akizungumza na  waziri Mukandara katikati  kushoto ni mkurugenzi wa maendeleo ya michezo Tanzania Bw,Leonard Thadeo 
..................................................................
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dk. Fenella Mukandara azungumza na  wanahabari mchana  huu ikiwa ni  pamoja na kueleza mafanikio ambayo serikali  ya  Rais Jakaya  Kikwete  imeyapata  katika  ziara yake na Rais nchini Uingereza.

Mbali ya  kueleza  kusudio la  wahisani wa klabu ya  Sanderland kuja  kujenga Academy ya mpira wa miguu kupitia kampuni ya Symbion Power ya Marekani nchini Tanzania kama  njia ya  kukuza  michezo hapa nchini bado amesema kuwa  ujenzi  wa Academi hiyo utafanyika ndani ya  jiji la Dar es Salaam  ama  Kibaha na kumpongeza mbunge wa  jimbo la Ilala ambae  alianza  jitihada za kuomba msaada  huo .

Pia  waziri  huyo  amewataka  wabunge  nchini  kuendelea  kupigania  ujenzi  wa  viwanja vya michezo  katika maeneo yao  pamoja na kuiga mfano  wa mbunge wa  jimbo  la Ilala mhe. Zungu katika kuwawezesha  kupata viwanja vya kidongo chekundu

Kuhusu mchezo kati ya Taifa  Stars  Ivory Coast waziri  huyo  alisema 
anaipongeza  timu  hiyo kwa mchezo  wake wa  jumapili na  kuwa mbali ya  kufungwa ila bado timu  hiyo ilionyesha soko na kuwa serikali itaendelea  kuiunga mkono




TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU UJENZI WA ACADEMY YA MPIRA WA MIGUU HAPA NCHINI

§  Kama mnavyofahamu, hivi karibuni Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alikuwa katika ziara yake ya kikazi nchini Uingereza.

§  Mhe. Rais alipokuwa nchini Uingereza alitembelea Club ya Sunderland. Mhe. Rais alihahidiwa kujengewa Academy ya Mpira wa Miguu na Kampuni ya Symbion Power ya Marekani ambayo itashirikiana na Club ya Sanderland katika kuindesha.

§  Hiyo Academy tunategemea itawezesha clubs zetu kupata wachezaji walio bora na walioandaliwa kuwa wachezaji wa taifa na kimataifa na hivyo kuboresha timu yetu ya Taifa na kuendelea kukuza muamuko wa masuala ya mpira wa miguu nchini.

§  Tunatarajia suala hili litafanyika na kutekelezwa mapema iwezekanavyo

§  Katika mpango  huo, Kampuni ya Symbion pia itajenga viwanja vya michezo (sports courts) pale Kidongo Chekundu. 

§  Kutokana na umuhimu wa suala hili, viongozi wakuu wa Kampuni ya Symbion wanatarajia kuja hapa nchini na nitakutana nao kwa ajili ya makubaliano mbalimbali na maandalizi ya utekelezaji.

§  Hivi sasa kama Serikali tunatafuta sehemu itakayojengwa Academy hiyo.  

§  Matarajio au nia yetu ni kujenga Academy hiyo Dar es Salaam au maeneo yaliyo karibu na Dar es Salaam.

§  Napenda nichukue fursa hii kumshukuru sana Mh. Rais kwa kufanikisha suala hili.

§   Napenda pia kumshukuru Mbunge wa Ilala Mhe. Mussa Zungu Azzan kwa kuwezesha kupatikana kwa viwanja vya Kidongo Chekundu.

 §  Napenda pia kutumia fursa hii kuwapongeza na kuwashukuru vijana wetu wa timu ya Taifa ”Taifa Stars” kwa juhudi na mchezo mzuri waliouonyesha wakati wa mechi yao na Timu ya Taifa ya Ivory Coast jumapili iliyopita.  Tupo pamoja nao na tutaendelea kuhakikisha tunawajengea uwezo zaidi ili waweze kupata mafanikio makubwa huko mbeleni.

§  Huko tunakoelekea, Academy itakuwa chimbuko la kupata wachezaji wazuri wa timu ya Taifa.
 

Asanteni kwa kunisikiliza

MWANDISHI WA CHARLES HILILA WA CHANEL TEN SHINYANGA AFARIKI DUNIA LEO

Aliyekuwa Mwandishi wa habari wa Kituo cha Channel ten Bw.Charles Hilila amefariki dunia  saa saba usiku katika Hospitali ya mkoa wa Shinyanga ambako alikuwa amelazwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu ya homa ya Malaria iliyokuwa ikimsumbua kwa muda wa siku chache zilizopita...MUNGU AILAZE MAHALI PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU CHARLES HILILA ,AMENI 

WAUZA MAGAZETI POSTA DAR WAWAHENYESHA MGAMBO WA JIJINI KATIKA SAFISHA JIJI RAIS OBAMA APITE

Wafanyabiashara  wa  magazeti  jijini Dar eneo la POsta mpya  wakiwa wamerejea  eneo hilo mbali ya kufukuzwa na mgambo  wa  jiji kutokana na zoezi la kusafisha  jiji hilo ili kujiandaa kwa ujio  wa Rais wa Marekan Barack Obama ,biashara  zote  eneo hilo zimepigwa marufuku na maeneo mengine ambayo msafara  wa Obama utapita
 



UJIO WA RAIS OBAMA TANZANIA WAWATESA MACHINGA NA WAUZA MAGAZETI POSTA

Rais Barack Obama wa Marekani  akisalimiana na Rais  Jakaya  Kikwete alipotembelea nchini Marekani hivi karibuni
Rais Obama
Hali  ilivyo kwa  sasa  eneo la Posta  mpya  jijini Dar es Salaam baada ya wafanyabiashara  ndogo ndogo machinga  na  wauza magazeti na vocha  eneo  hilo  kuondolewa na mgambo  wa  jiji katika zoezi la kusafisha jiji kwa ajili ya ugeni  huo mkubwa nchini

.....................................................

ZIKIWA zimebaki  siku chache kabla  ya  Rais  wa Marekani Barack Obama  kufanya  ziara  yake chini Tanzania ,wafanyabiashara  ndogo ndogo maarufu kama Machinga na  wauza magazeti na  vocha eneo la Posta mpya  jijini Dar es Salaam  wamedai  kunyanyasika na mgambo  wa  jiji kupitia msako mkali unaofanyika .
Msako  huo  umeanza mapema asubuhi ya  leo katika  eneo hilo la Posta na maeneo mbali mbali ya jiji la Dar es Salaam ambako msafara wa Rais Obama utapita kutokea  uwanja  wa kimataifa  wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere kuelekea Ikulu ya Dar es Salaam 

Wakizungumza na mtandao  huu wa www.matukiodaima.com baadhi ya  wafanyabiashara  hao ambao wamelazimika  kusitisha shughuli za biashara  zao  eneo  hilo ,wamesema  kuwa mbali ya ujio  huo  wa Rais Obama nchini  kuwa ni heri kwa Taifa  ila kwa upande  wao wanapinga hatua ya mgambo  kuwanyanyasa kwa  kuwatimua  eneo hilo ambalo  siku  zote  wamekuwa wakifanya kazi na mbaya  zaidi  wameamua kuwatimua hadi  wauza magazeti .

 Alisema mfanyabiashara  Ally Husein  kuwa  kutokana na siku ya  ziara ya Rais Obama  kuwa bado kama  takribani siku 12 mbele  ni  vema uongozi  wa jiji na mkoa  wa Dar es Salaam ukatumia busara  zaidi kwa  kuwaacha kwa  siku hata 7 mbele ama tano  ili  waendelee na biashara kwa ajili ya  kujitafutia mahitaji yao ya  kila  siku kuliko kuwazuia kuanzia leo .

"Kweli  ujio  huu  wa Rais Obama  unatutesa  sana  sisi  walalahoi ambao tunategemea  kuendesha maisha  yetu kwa kuwepo hapa Posta kwa kufanyabiashara za kuuza magazeti na vocha.....Serikali ya mkoa  wa Dar es Salaam tunaomba ilitazame kwa undani  zaidi suala  hili la kutulaza njaa kwa siku zote 12 bila kufanya shughuli"

Hata  hivyo alisema  kuwa  idadi kubwa ya  wafanyabiashara  eneo hilo wamekuwa wakiendesha biashara  zao kwa kupitia mikopo hivyo kuzuiwa kwa muda  wote  huo kutawaharibia mwelekeo  wa kimaisha  .

Hivyo  alishauri  serikali kuwa katika maandalizi ya  ujio  wa Rais  Obama nchini  bado  kutumia njia nzuri ya  kuweka  jiji  safi pasipo kuwaumiza  wananchi  wenye  kipato cha chini wanaofanya  shughuli zao katika eneo hilo.

"Hivi kama  siku  zote  tumekuwa  tukiuza magazeti katika eneo hilo na hakukuwa na uchafuzi  wowote wa mazingira  leo serikali inatuondoa eneo hili na kutuona kama ni uchafu ....kweli katika  hili ni  kutunyanyasa  wanyonge "
 KWA UDHAMINI WA SHABIBY BUS LINE  NI USAFIRI  WA  UHAKIKA NA  SALAMA KABISA NA  HOPE SERVICE STATION IRINGA



Abiria  wakiwa  ndani ya basi la Shabiby Line ambalo ni  Full Luxury lenye  choo ndani na  huduma  nyingine  zote ndani

HOPE SERVICE STATION HAPA HUDUMA NI MASAA 24

 Wengi  hukimbilia  kununua mafuta hapa HOPE SERVICE STATION eneo la CRDB barabara ya Iringa -Dodoma katikati ya mji  wa Iringa  kituo  kinachouza mafuta masaa 24 ,wewe wasumbuka na nini  jiunge  na kituo  cha  wengi  sasa .