September 22, 2012

MSIMAMO WA WANAHABARI IRINGA DHIDI YA WIKI YA NENDA KWA USALAMA,ILI KUWA NI RADIO COUNTRY FM ,LEO NI EBONY FM AMA NDIO MKUKI KWA NGURUWE?

Mwenyekiti  wa kamati ya  wiki ya nenda  kwa  usalama barabarani mkoa  wa Iringa  Salim Abri Asas akipokea cheti toka kwa waziri  wa mambo ya ndani ya nchi Dkt Emmanuel Nchimbi (kulia) wakati  wa uzinduzi  wa maadhimisho hayo.

Hakika kama ni msimamo  wa wanahabari mkoa  wa Iringa kutoshirikiana na jeshi la  polisi katika  kuripoti matukio mbali mbali ya  wiki ya nenda  kwa  usalama iliyofanyika  kitaifa katika  viwanja  vya  Samora mjini Iringa ,umeyumbishwa  kweli kweli na vituo vya radio ama kumekuwepo na lugha gongana kwa  wanahabari hao.

Siku  mbili zimepita toka kituo  cha radio Counrty Fm Iringa  kiliposhambuliwa  kwa  kurusha matangazo ya  moja kwa moja  kutoka uwanja  wa samora katika maadhimisho hayo kwa madia  kuwa kilikiuka makubaliano ya pamoja  yaliyowekwa na  wanahabari  katika  kususia  kushirikiana na jeshi la  polisi na hata  kutuhumiwa  kuhongwa  pesa ili  kusaliti msimamo  huo jambo ambalo Bw Temy Mahondo  aliweza  kutolea  ufafanuzi  kuwa wao  walipokea fedha kwa ajili ya matangazo sio vinginevyo.

Leo tena  tunashuhudia  kituo  cha radio Ebony Fm cha Iringa  pia kinaingia katika kundi kama hilo la kusaliti mshikamano wa  wanahabari Iringa kwa  kurusha tena kwa uzito  zaidi maadhimisho hayo hali ambayo imenifanya kama kiongozi  wa IPC  kupigiwa  simu  nyingi  sana na  wanahabari wakihoji juu ya radio  Ebony Fm  kusaliti pia msimamo  wetu .

Nasema  kwa bahati mbaya  wakati napigiwa  simu kuwa  sikiliza online  radio Ebony kweli  nilikuwa  mbali na Laptop yangu sikuweza  kusikiliza ila kama  ni kweli radio Ebony Fm wamerusha maadhimisho hayo nategemea  ushirikiano  walioonyesha  siku Radio  Counrty Fm ilivyotangaza maadhimisho  hayo ndivyo ambayo leo  watanipigia  simu  mimi ama  katibu  wangu Frank Leonard aliyeko huko Ili  kuelezea  suala  hilo .

Katika  hili lazima utolewe  ufafanuzi kwa  wanahabari wote  kama tumeamua kusitisha msimamo na kuamua  kuendelea  kufanya kazi na jeshi la  polisi ni lazima ijulikane vinginevyo hakukuwa na haja ya  kuweka msimamo kufuatia  kifo cha Daudi Mwangosi .

Upo usemi unaosema  kuwa mdogo akichukua mboga nyingi  zaidi hulalamikiwa na hata  kuadhibiwa kwa  kudaiwa  kukomba mboga na mkubwa akifanya  hivyo kwake ni kawaida nachotaka kusema hapa radio zote ni sawa na vyombo  vyote ni  sawa lazima msimamo uwe kwa  vyombo vyote na  wanahabari wote .

Naendelea  kuwasiliana na katibu  wangu  ili kutoa tamko katika  hilo kupitia  wanahabari wote  bila kujali ni mwanachama ama si mwanachama  wa IPC kiukweli nimevunjika moyo kabisa kwa yanayoendelea  kutokea Iringa

Huu ni mtazamo  wangu na si msimamo  wa IPC naomba ieleweke  hivyo

3 comments:

Anonymous said...

Ninasikitika sana kuona Wanahabari mpo katika Mgomo!

Sisi wananchi tilitegemea kupata elimu ya usalama barabarani kupitia vyombo vya habari, lakini mgomo wenu umesababisha tukose habari muhimu. Tunashukuru sana Blogs ambazo zilikuwepo Iringa kwaajili ya kuhabarisha umma juu ya Maadhimisho hayo. Hivi niwaulize Waandishi wa Iringa inapotok ajali ni polisi wangapi hufa au ni sisi wananchi? Wananchi tupo mbioni na sisi kugomea taarifa zenu hasagazeti.

Nawapongez walio ripoti tukio

Anonymous said...

kweli pesa kitu kibaya sana hata Yuda alimsaliti yesu, kwa hili sina imani tena na hao wanaojiita watangazaji.

Anonymous said...

Msipumbazwe na wanachokifanya hao jamaa zetu wa FM Radios za hapo Iringa!Endeleeni na msimamo wenu.Siku ikifika ya kusitisha mgomo,basi,mtalitolea tamko,na ulimwengu utawaelewa nini mlichokusudia kufanya!Asiye na akili timamu tu ndiye atakayeshindwa kuelewa ujumbe wenu ulikuwa na maana gani katika jamii!Viva IPC!